Thursday, June 27, 2013

TRA:Kodi ya magari kulipwa kwa kwa njia ya mtandao kuanzia 1'Julai



Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kushirikiana na Benki kuu ya Tanzania (BOT) wamefanya maboresho katika ulipaji kodi kwa njia ya mtandao.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi wa Fedha wa TRA Salehe Mshoro alisema kuanzia Julai mosi TRA na BOT  wataanzisha mfumo wa ukusanyaji kodi utakao unganisha na mifumo ya benki.kuu na benki za biashara.

Alisema kuwa mtu akienda kulipa kodi zile fedha zitakwenda BOT  na papo kwa hapo atapata taarifa kwa njia ya barua pepe  na taarifa zitakwenda kwa haraka TRA zitakazoonyesha kuwa kodi imelipwa.

Alidai kuwa mfumo huu utaondoa migongano ya mara kwa mara na pia watakuwa wamefanya  makubaliano kati ya TRA na wananchi ambao ndio walipa kodi.na pia mfumo huu wamejufanyia majaribu toka mwezi januari.

Aidha alisema mfumo huu utaanza kutumika kwa walipa kodi wakubwa wa malipo yanayoanzia millioni tano(5) ambao hao watakuwa mabalozi kwa wengine wadogo na alisema kumbukumbu zitaingizwa kwenye mamlaka na watapata taarifa.

Mlipa kodi atatakiwa kujisajili kwenye mtandao wa TRA ambao ni www.tra.go.tz akiingia kwenye wwbsite ya TRA anaweza kupata taarifa zake muhimu za usajili na namba za utambulisho na benki yake.


Naye Murugenzi wa mradi Ramadhani Sangeti alisema wamejiunga na mkongo mkubwa wa taifa  na endapo mkongo mkubwa hautapatikana ile mingine itasaidia,

Mategemeo ya TRA ni kuwa utaongeza urahisi wa ulipaji kodi na utaondoa kero za wananchi pia itapunguza muda na kumpunguzia mteja gharama, kwani ni mfumo salama wenye kutoa taarifa kwa wakati.

Mwisho aliwataka walipa kodi pindi watakapopata matatizo yoyote wapige namba za huduma ambazo ni bure  kwa upande wa TTCL na Vodacom ni 08001126 au Tigo ambazo n i 0713800333 na Airtel 0786800000

No comments:

Post a Comment