Monday, June 10, 2013

"Ningekuwa Ruge, Ningemwomba Radhi Jaydee"Asema Sebo


Mtangazaji wa kipindi cha Sun Downer cha Magic FM, Sebo amesema kwamba shangwe zilizolipuka mara baada ya Jaydee kutajwa kuwa miongoni mwa wanaowania tuzo ya msanii bora wa kike ktk tuzo za KTMA, ni ishara ya mwanadada huyo kukubalika ktk jamii. Mtangazaji huyo amesema kwamba Jaydee ni mwanamke mwenye uthubutu ktk harakati za kuyasaka maisha na kwamba yeyote mwenye nia ya kukwamisha jitihada zake aibu na iwe juu yake. Ameongeza kuwa kukubalika kwa mwanadada huyu pia kulidhihirika pale ambapo watazamaji ktk tukio hilo walipomshinikiza Meneja wa msanii huyo (Gadna) kutaja kiingilio na tarehe ya maadhimisho ya miaka 13 ya Jaydee ktk uga wa muziki. Hivyo, Sebo anaona ni vyema Ruge akajishusha na kumaliza tofauti zake dhidi ya Jaydee.

No comments:

Post a Comment