Friday, June 21, 2013

Matusi yachangia Stars kufungwa:Gadi



Simon Mmbando.
Askofu Charles Gadi wa kanisa la Good News for all Minister  amesema kuwa lugha ya udhalilishaji na matusi vilichangia kufungwa kwa timu ya Taifa Stars.

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo alisema ziposababu nyingi zilizo sababisha Taifa Stara kupoteza mchezo wake dhidi ya Ivory coast uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Askofu Gadi alisema sababu kubwa iliyopelekea Taifa Stara kupoteza mchezo wake ni Mizaha mingi ya washangiliaji na matusi yaliyokithiri ambayo mbele za Mungu huonekana kama sio maombi.

Unapo tukana Mungu husika kama vile akusikiapo unavyo omba hvyo sisi sote kama Watanzania tulimwamini Mungu na tukiamini tutapata ushindi. Ni jambo la ajabu kuona watu wanaomba msaada wa Mungu na wengine wanatukana matusi.

Hali hiyo hukinzana na Mungu na mwisho wake kushindwa kama hali hiyo ya matusi ikipitiliza ushindi kwetu itakuwa ni ndoto.

Aliendelea kusema kuwa goli la kwanza lilifungwa kwa maombi ya Watanzania waliokuwa pale na walio kuwa majumbani kwao wakiomba, lakini matusi yalio endelea ya kutukana maumbile ya siri ya Mama zetu,Wake zetu, Wakwe zetu, Dada zetu na Watoto wetu wa kike yalitukwamisha.

Matusi hayo yalikwamisha ushindi kwa Taifa Stara kwani unapo tukana maumbile ya akina mama ni sawa na kuchafua na kukejeli uumbaji wa Mungu kwa akina mama na hali hiyo hupelekea laana na hali ya kushindwa.

Alisema cha ajaba hakuna hatua zozote zinazochukuliwa na imefikia wakati tuziombe mamlaka usika hasaBunge na Wabunge na akina mama wasiyafumbie macho mambo hayo bali watunge sheria zenye kutoa adhabu kali kwa watu wenye mazoea ya kutamka matusi.

Kama zilivyo nchi nyingine kutema bigijii unaweza kufungwa miezi mitatu kwanini nch yetu unalifumbia macho kosa matusi Mabaya kama hayo au yanaonekana ni situ cha kawaida, utadhani Uwanjani pale palikuwa na kiwanda cha kuzalisha matusi.

Hali hiyo ya matusi inachafua sura nzima ya tasnia ya michezo  na itatufanya tuwe wasindikizaji kwani mambo haya yana athari sana katika ulimwengu wa roho na yasipo tiliwa mkazo kuna uwezekano wakuwa poteza maajenti ambao huja nchini kutafut wachezaji na kuwauza nje ya nchi.

Kuhusu usalama kwa watazamaji alisema uwanja ulijaa kwa kiwango ambacho ni tatizo kama kukitokea jambo la hatari kwani watu walijazana hadi njia za lupita watu, wanaishauri serikali iweke screen kubwa nje ya uwanja ili kwa watakaochelewa
Kuingia uwanjani waangalie mpira lupita nje ya uwanja.

Taifa Star ilicheza mchezo huo dhidi ya Ivory coast Juni,16 mwaka huu na  kupoteza kwa kufungwa magoli 4-2 na kupoteza nafasi yakushiriki kombe la dunia litakalofanyika  nchini Brazil Juni, mwakani.


Mwisho alitoa pongezi kwa Wachezaji, Serikali,Wananchi, TFF na kamati (Saidia Taifa Star Ishinde) kwajitahada walizofanya katika maandalizi ya timu yetu, pia wakazi wote wa Dar es Salaam na wote waliofika uwanjani kwani walionyesha uzalendo wa kuipenda nchi yao.

No comments:

Post a Comment