Monday, June 10, 2013

Monday, June 10, MARA BAADA YA TAIFA STARS KUREJEA-POULSEN ANENA NA KUSEMA WANGEKUWA WANGECHEZA 11 UWANJANI WASINGEFUNGWA NA,MOROCCO


Kocha wa Timu bali matokeo ya Taifa (Taifa Stars), Kim Poulsen amesema refa wa mechi ya Taifa Stars na Morocco iliyopigwa Marrakech Jumamosi kusaka tiketi ya kucheza fainali za Kombe la  Dunia Brazil mwakani aliuwa mchezo kwa kutoa kadi nyekundu kwa mchezaji Aggrey Morris.
Akitoa maoni ya mchezo huo, Poulsen alisema alisikitishwa na jinsi refa huyo alitoa adhabu kali ambayo haiendani na kanuni za FIFA.
Aggrey Morris alioneshwa kadi nyekundu baada ya kugongana na Abderazak Hemed Allah ambaye aliifungia Morocco bao la kwanza katika dakika ya 37.
“Hakuwa na sababu ya kumuonesha Morris kadi nyekundu kwani tayari alishawapa Morocco penalti, alisema Poulsen huku akiongeza, “FIFA imeshawaonya marefa mara kadhaa dhidi ya kuua mchezo kwa namna hii ya kutoa adhabu kali kupita kiasi.”
Poulsen alisifu wachezaji wake na kusema licha ya kucheza pungufu walipambana uwanjani na kufanikiwa kupata bao kupitia kwa Amri Kiemba. Morocco walishinda kwa 2-1.
“Kama tungecheza kumi na moja hadi mwisho nina uhakika tungeshinda mechi hii lakini refa aliiua mechi na huwezi kufanya hivi katika mechi ngumu kama hii,” alisema Poulsen.
Kocha huyo alisema kupata goli la ugenini unapochez na timu ngumu kama Morocco ni jambo la kujivunia hasa mnapokuwa pungufu uwanjani.
Alisisitiza kuwa sasa wanaelekeza nguvu zote katika mechi shidi ya Ivory Coast Jumapili ijayo. “Mambo ya Morocco yamekwisha sasa tunafikiria namna ya kushinda mechi ya Jumapili.
Tanzania iko katika kundi C inayoongozwa na Ivory Coast yenye pointi 10, Tanzania 6, Morocco 5 na Gambia 1.
Taifa Stars imerejea Jumatatu alfajiri kutokea Marrakech Morocco na itaendelea na kambi ya wiki moja ili kujiandaa na mechi dhidi ya Ivory Coast.
Nahodha wa Taifa Stars, Juma Kaseja alisema wachezaji walicheza kwa ari kubwa na walifurahishwa na jinsi watanzania walijitokeza kwa wingi.
“Tulipata faraja kubwa sana kuwaona watanzania wengi uwanjani…mambo ya Morocco yameisha sasa tuangalie Ivory Coast,” alisema.
Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe ambaye bia yake inadhamini Taifa Stars, alisema wacezaji walijitahidi hasa ikizingatiwa walicheza pungufu na hata wakafanikiwa kufunga bao moja.
“Katika hali kawaida, wachezaji wengine wangekata tamaa lakini bao hili moja linaonesha kuwa wachezaji walikuwa na ari ya kupata ushindi,” alisema Bw Kavishe.
Alisema wao kama wadhamini wana imani kubwa na Taifa Stars na kwamba wanaamini hii ni safari ya mafanikio ambayo ilianza mwaka mmoja uliopita tangu Bia ya Kilimanjaro Premium Lager ianze udhamini huo.

Chadema yakubali Serikali tatu


Mbeya/Dar. Mwenyekiti wa Chadema, Freeman ameweka bayana kuwa wanaunga mkono Rasimu ya Katiba na hasa suala la Muungano wa Tanzania kuundwa na Serikali tatu kama ilivyopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
 
Mwenyekiti wa Chadema, FreemanMbowe
Amesema mambo mengi yaliyopendekezwa na chama chake yamefanyiwa kazi na Tume ya Mabadiliko na kuishangaa CCM akidai kwamba inapinga rasimu hiyo hususan suala la Serikali tatu wakati kimsingi watu wa Tanzania Bara wamekuwa wakipunjika kwenye muundo wa sasa wa Muungano.
 
Akihutubia mkutano wa kampeni ya kuwania udiwani wa Kata ya Iyela katika Uwanja wa Bongonela, Mbeya jana jioni, Mbowe alisema chama chake kinataka kuona Serikali ya Tanganyika ikifufuliwa. Alikuwa akimnadi mgombea wa Chadema, Charles Mkela.
 
Alisema Chadema kinataka kuona Wazanzibari wakiwa na Serikali yao ili wajiamulie mambo yao na pia Watanganyika wawe na uongozi wao lakini waunganishwe na Serikali ya Muungano.
 
Alisema muundo wa sasa wa Muungano una matatizo. Kwa mfano, mbunge wa Zanzibar anawakilisha watu wachache zaidi ukilinganisha na mbunge wa Bara. Wananchi mtashangaa sote tunalipwa sawa.”
 
“Ila zikija Serikali tatu ina maana kuwa kila upande wa Muungano utatumia rasilimali zake. Haya mambo kulipana fedha nyingi kwa kazi kidogo yatakoma.”

Saturday, June 8, 2013

Kunauwezekano wa kugawanywa ikulu ya rais:Warioba

Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba nchini Tanzania, Jaji Joseph Warioba amesema iwapo Mfumo wa Serikali Tatu utaridhiwa na wananchi ni lazima mambo yaliyo ndani ya Muungano yatagawanywa ikiwa ni pamoja na Ikulu ya Rais. Amesema kutokana na taifa kufanya mabadiliko ya Katiba ni lazima kuwepo mpangilio wa kugawana mambo mbalimbali yaliyokuwa chini ya Muungano ikiwamo majengo, wafanyakazi, Ikulu, hata vitendea kazi na kwamba utaratibu huo ni kama ule uliotumika wakati Tanganyika na Zanzibar zilipoungana. Kauli ya hiyo ya Jaji Warioba imekuja siku tatu tangu Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe kueleza kuwa Tanzania Bara itaanza mchakato wa kutunga Katiba yake Aprili mwaka 2014 na kumalizika Desemba mwaka huohuo. Jaji Warioba aliyasema hayo katika mahojiano maalumu na waandishi wandamizi wa habari jijini Dar es salamu, Tanzania. Hata hivyo aliongeza kuwa suala hilo linahitajia mazungumzo ya pande zote mbili, baada ya kukamilika kwa mchakato huu kwa sababu hii ni rasimu tu, ambayo itajadiliwa na wananchi kabla ya kuanza kwa Bunge la Katiba na baadaye kuwepo kwa kura ya maoni.

Cesc Fabregas azigombanisha Man United na Arsenal.

Klabu za Manchester United na Arsenal zimeingia kwenye vitakali ya kuwania saini ya kiungo wa kimataifa wa Hispania Cesc Fabregas anawaniwa na klabu za Manchester United na Arsenal baada ya klabu yake ya Fc Barcelona kudaiwa kuwa tayari kusikiliza ofa kwa ajili yake .
Fabregas ambaye alicheza nchini England kwenye klabu ya Arsenal kwa muda wa miaka nane ameshindwa kufikia kiwango kilichotarajiwa na Barcelona wakati inamnunua toka Arsenal na kwa sasa iko tayari kumuuza ili kutengeneza fedha za kununua mchezaji mwingine .
Kocha mpya wa Manchester United David Moyes amegundua kuwa United ina tatizo kwenye safu ya kiungo na yuko tayari kuidhinisha paundi milioni 40 kumnunua Cesc , hata hivyo Arsenal ndio wenye haki ya kwanza ya kuzungumza na kiungo huyo kwa mujibu wa makubaliano baina ya Barca na Arsenal wakati wa mauzo yake toka London kwenda Hispania na endapo watakuwa tayari kumnunua basi Unitd wanaweza kupoteza nafasi ya kumsajili.
Kwa upande mwingine kocha wa Arsenal Arsene Wenger hapo jana alianza rasmi mchakato wa usajili kwenye kikosi chake baada ya kutuma ofa ya paundi milioni 22 kwa ajili ya kiungo wa Everton Marouanne Fellaini .
United nao wanajiandaa kumthibitisha beki wa timu ya taifa ya Uruguay kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20 na klabu ya Penarol Guillermo Varela ambaye alithibitisha mwenyewe kufanyiwa vipimo vya afya huko Manchester.

ASILIMIA 15 YA MAPATO YA SHOW YANGU YA "THE FINEST" NITATOA KWA MAMA WA MAREHEMU NGWEA:MWANA FA

FA: ASILIMIA 15 YA MAPATO YA SHOW YANGU YA "THE FINEST" NITATOA KWA MAMA WA MAREHEMU MANGWEA.

 



Baada ya show ya Mwana FA "The Finest" Kuahirishwa wiki iliyopita kutokana na msina wa Rapper Abert Mangwea, aliyefariki jumanne ya tarehe 28 May na kuzikwa siku ya jana Morogoro,
Kama Zamani The Finest,Imetangazwa tena, na safari hii asilimia 15 ya mapato kutoka katika show hiyo, yatapelekwa kwa mama mzazi wa Ngwea.

"nimesema kwamba nitoe hela mfukoni kwangu moja kwa moja, niipeleke huku, kwahiyo chochote nitakacho kipata, nataka kutoa 15 percent nimpelekee bi mkubwa...."amesema Fa

"unajua kitu kama cha kumuita ngwea marehem,  bado kilikuwa hakija click kichwani kwangu, hakiji, yaani watu wakimuitwa mangwea marehem naona aaaah, hawa jamaa wanasema vitu gani, bado inanisumbua "

" Nafkiri Pengine sikufanya vyakutosha wakati yuko hai, lakini bado naweza kufanya kitu kama anaona huko aliko naomba awe na moyo mwepesi na mimi, nimeona ntamuandali hiki ambacho nakipata sasa hivi, nimuangalie mama yake, kama ambavyo pengine yeye angefanya kama ingekua album yakwake.amesema mwana FA.

POULSEN AHAIDI SOKA LA KASI KATIKA MECHI DHIDI YA MOROCCO NAYE KASEJA ASEMA HAWAIOGOPI MOROCCO ILA WANAIHESHIMU




Marrkech, Morocco
Huku Timu ya Taifa Taifa Stars ikikabiliwa na mechi muhimu kesho (Jumamosi) dhidi ya Morocco kusaka tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia, Kocha Kim Poulsen amesema amejiandaa kucheza mpira wa kasi na wenye pasi za uhakika ili kuivuruga beki ya Morocco.
Kocha huyo ameyasema hayo katika mkutano na waandishi wa habari na kusisitiza kuwa ni muhimu kuhakikisha Morocco hawaupati mpira kwa urahisi.
“Wachezaji wako katika hali nzuri kabisa na wana ari ya kushinda mechi hii…tuna nguvu na tunajua namna ya kuwapiga Morocco,” alisema kocha huyo.
Alisema suala si mchezaji gani anaanza au washambulizi ni wangapi, bali ni kazi itakayofanyika uwanjani na ubora wa wachezaji wa Taifa Stars, inayofurahia udhamnini mnono wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager.
Alisema Morocco ni timu kubwa na ina wachezaji wengi wa kulipwa lakini inafungika na Taifa Stars itaweka nguvu kuanzia mwanzo wa mechi.
“Unapocheza mechi kama hii inabidi uweke nguvu dakika za kwanza za mechi ili umpe mpinzani wakati mgumu kwa hivyo dakika za mwanzo zitakuwa muhimu sana katika mechi hii,” alisema.
Poulsen alisema baadhi ya watu nchini Morocco bado wanaamini kuwa ushindi wa mechi ya awali Jijini Dar es Salaam wa 3-1 dhidi ya Morocco ulikuwa wa kibahati tu. “Tunataka kuwadhihirishia kuwa tunaweza na Taifa Stars sio timu ndogo kama wanayodhani.”
Alisema mazingira ya kambi ni mazuri kabisa na wachezaji wote wako katika hali nzuri na tayari kwa mchezo huu.
“Katika hali ya kawaida ungetegemea hujuma nyingi ikiwemo hoteli mbovu, viwanja vibovu vya mazoezi na kadhalika lakini hapa ni tofauti kabisa…kwani mazingira ni mazuri,” alisema Poulsen.
Taifa Stars imeweka kambi katika Hoteli ya Pullman iliyoko nje kidogo ya Mji wa Marrakech.
Naye nahodha wa Taifa Stars, Juma Kaseja alisema wamefanya mazoezi ya kutosha hasa ikizingatiwa kambi ilianzia Addis Ababa, Ethiopia ambako walicheza mechi ya kirafiki na Sudan na kutoa sare ya 0-0 kabla ya kuelekea Marrakech.
“Morocco ni timu kubwa, tunapaswa kuiheshimu lakini sio kuiogopa…tutapambana ili timu ipate matokeo,” alisema Kaseja.
Naye Meneja wa Bia ya Kilimanajro Premium Lager, George Kavishe, akizungumza kutoka Dar es Salaam alisema wao kama wadhamini wa Taifa Stars wana imani kubwa sana na Stars na wanaitaka iwape Watanzania raha kwa mara nyingine kwa kushinda mechi hiyo.
“Tumewaona wakifanya vizuri nyumbani kwa kushinda mechi tano mfululizo na sasa ni muda wa kupata ushindi nje,” alisema.
Stars iko katika kundi C pamoja na Ivory Coast, Morocco na Gambia. Kundi hilo linaongozwa na Ivory Coast yenye pointi 7, Tanzania 6, Morocco 2 na Gambia 1.
Mechi ya kesho itapigwa katika Uwanja wa Marrakech saa tatu usiku kwa saa za Morocco ambayo itakuwa saa tano kamili Tanzania.
Baada ya Morocco Stars itacheza na Ivory Coast nyumbani Jumapili ijayo na mechi ya mwisho itakuwa dhidi ya Gambia Septemba mwaka huu.

Thursday, June 6, 2013

TANZANIA YAPAA VIWANGO VYA UBORA VINAVYOTOLEWA NA FIFA

USHINDI wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars waliopata katika mchezo wa kufuzu michuano ya Kombe la Dunia 2014 dhidi ya Morocco umesaidia kuipandisha nchi katika viwango vya ubora wa soka duniani.

Katika orodha hizo za kila mwezi zilizotolewa leo Tanzania imekwea kwa nafasi tatu kutoka nafasi ya 119 waliyokuwepo mwezi uliopita mpaka nafasi ya 116 hivyo kuendelea kufanya vyema ukilinganisha na mwaka jana. 

Mabingwa wa Dunia na Ulaya, Hispania wameendelea kung’ang’ania kileleni mwa orodha hizo wakifuatiwa na Ujerumani katika nafasi ya pili na Argentina katika nafasi ya tatu huku kwenye nafasi ya nne kukiwa na ingizo jipya la nchi ya Croatia waliopanda wa nafasi tano mpaka kufikia ya nne na tano bora inafungwa na Ureno.

Kwa upande wa Afrika, Ivory Coast wameendelea kushika nafasi ya kwanza baada ya kupanda kwa nafasi moja duniani mpaka nafasi ya 12 wakifuatiwa na Ghana katika nafasi ya pili ambao wao wamedondoka kwa nafasi mbili mpaka ya 22 duniani. Mali wao wako nafasi ya tatu wakifuatiwa na mabingwa soka barani Afrika Nigeria katika nafasi ya nne na tano bora Algeria.inafungwa na