Friday, July 5, 2013

Sumaye azindua ziara Dsj



 Posted on 5jully 2013
Waziri mkuu mstaafu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Fredrick Sumaye amezindua safari ya kuelekea nchini Kenya ya wanafunziwa chuo cha uandishi wa habari Dar es Salaam (DSJ).na kuwataka kutumia fursa hiyo kuitangaza zaidi Tanzania

Sumaye amezindua safari hiyo chuoni hapo na kuwataka wanafunzi kwenda kujifunza utalii na jinsi ya kumudu maisha pasipo kutegemea kuajiriwa na serikali bali kujiajiri wenyewe kwa elimu waliyoipata.

Pia aliwataka wanafunzi hao kujifunza mazingira ya Kenya jinsi yalivyo tofauti na ya hapa kwetu Tanzania na hata watalii wengi huvutiwa   kutembelea  nchi hiyo na  kuwaongezea pato lao la taifa.

Alisema kuwa nchi ya Kenya iko juu kiuchumi tofauti na Tanzania  hivyo  basi    mnavyokwenda ni vizuri mkajijifunze kutoka kwa wenzetu na kuja kuyafanyia kazi kwa ufasaha zaidi ili kuleta maendeleo  kwa taifa Letu.

Sumaye aliendelea kusema wafanyakazi wa Kenya ni wafanyakazi waamifu  na wachapa kazi sana tofauti na Tanzania hivyo basi nasi  tukajifunze vitu hivyo katika ziara hii ili tuweze kulijenga taifa letu.

Kwa upande wa biashara alisema Kenya wanauwezo mkubwa wa kufanya biashara za nje tofauti na Tanzania hivyo nasi tukaifunze mbinu hizo za kibiashara kutoka kwao ili tuje kuwa mabalozi hapa nchini..

Ziara hiyo inatarajiwa kuwa ya siku tano kuanzia taehe 9 mwezi wa saba hadi tarehe 14 ambapo malengo ya ziara hiyo ni kujifunza utamadunui wa nje pamoja na kujifunza elimu yao ilivyo tofauti na Tanzania.

No comments:

Post a Comment